Rais Jacob Zuma wa Afrika kusini amemfukuza kazi mkuu wa polisi nchini humo. Bheki Cele alifukuzwa kazi jana katika hatua ambayo ni nadra kuchukuliwa dhidi ya afisa wa ngazi ya juu anayetuhimiwa kwa rushwa.
Rais Zuma aliuambia mkutano na waandishi habari mjini Pretoria kwamba ameamua kumsimamisha kazi Jenerali Cele, na wakati huo huo akatangaza mageuzi madogo ya baraza lake la mawaziri.
No comments:
Post a Comment