Saturday, June 30, 2012

ARMSTRONG AFUNGULIWA MASHITAKA YA KUTUMIA DAWA ZA KUONGEZA NGUVU.

Lance Armstrong.
BINGWA mara saba wa michuano ya baiskeli ya Tour de France, Lance Armstrong amefungiliwa mashtaka ya kutumia dawa za kuongeza nguvu na wakala wa kupinga dawa hizo nchini marekani. Kesi hiyo sasa itasikilizwa na jopo la kamati ya upatanishi ambalo litaamua matokeo ya kusikilizwa kwa kesi hiyo. Armstrong ambaye alishinda michuano hiyo mara saba mfululizo kuanzia mwaka 1999 mpaka 2005 anaweza kunyang’anywa mataji yake hayo na kufungiwa kushiriki mbio za baiskeli kama akikutwa na hatia ya kutumia dawa hizo. Hatahivyo Armstrong ambaye ana umri wa miaka 40 alikana tuhuma hizo na kudai kuwa hakuwahi kushindwa katika vipimo vya dawa za kuongeza nguvu katika kipindi chote ambacho amekuwa akishiriki mbio hizo.
Armstrong ambaye alifanikiwa kupona kansa ya korodani na kufanikiwa kuweka rekodi ya michuano hiyo ya Ufaransa alistaafu mbio hizo mwaka 2005 lakini alirejea tena mwaka 2009 kabla ya kustaafu kwa mara ya pili Februari mwaka 2011.

No comments:

Post a Comment