Saturday, June 30, 2012

PRANDELLI AANZA KUSHEHEREKEA UBINGWA.

KOCHA wa timu ya taifa ya Italia Cesare Prandelli ameonekana akijipongeza na maofisa wa soka wa nchi hiyo baada ya kuitoa Ujerumani katika hatua ya nusu fainali ya michuano ya Ulaya na kufanikiwa kutinga fainali ambapo watakutana na Hispania kesho jijini Kiev, Ukraine. Katika tafrija hiyo ndogo Prandelli amesema kuwa anafurahia changamoto ya kumfundisha mshambuliaji mtukutu wa timu hiyo na klabu ya Manchester City Mario Balotelli na wamekuwa wakielewana vizuri katika michuano hiyo mpaka sasa. Mwanzoni kabla ya kuanza kwa michuano hiyo kulikuwa na tetesi kuwa Prandelli angemuacha Balotelli kutoka na tabia za utovu wa nidhamu ndani na nje ya uwanja ambapo baada ya kumwita katika kikosi chake wadau walikuwa wakiuliza kama kocha huyo ataweza kummudu mchezaji huyo mtukutu. Prandelli alitamba kuwa mbali na kumfundisha Balotelli pia amewahi kuwafundisha wachezaji kama Adriano, Antonio Cassano na Adrian Mutu ambao ni watukutu lakini mwisho wa siku ndio wamekuwa wachezaji ambao huibuka kuwa nyota ya mchezo tofauti na watu wanavyowategemea.

No comments:

Post a Comment