Saturday, June 30, 2012

VILLAS-BOAS KUPOTEZA KIASI CHA PAUNDI MILIONI 11 KAMA AKITUA WHITEHART LANE.

ALIYEKUWA kocha wa Chelsea Andre Villas-Boas anatarajiwa kupoteza kiasi cha paundi milioni 11 kama atatangazwa kama meneja mpya wa kikosi cha Tottenham Hotspurs wiki ijayo. Kocha huyo raia wa Ureno mwenye umri wa miaka 34 hajapatiwa malipo yake wakati alipofukuzwa na Chelsea Machi mwaka huu akiwa ametumikia miezi nane katika miaka mitatu ya mkataba huo. Badala ya kulipwa moja kwa moja fedha hizo Chelsea walikubali kumlipa kocha huyo kiasi cha paundi 100,000 kwa wiki mpaka hapo atakapopata kibarua kingine ambapo alikuwa amepokea mshahara wa miezi mitatu tu. Lakini kama kocha huyo akiamua kukubali kuinoa klabu ya Tottenham, tajiri wa Chelsea Roman Abramovic atasitisha malipo ya kocha huyo ambayo amekuwa akipata hivyo kupoteza kiasi cha paundi milioni 11 katika miezi 25 iliyobakia.

No comments:

Post a Comment