Friday, June 29, 2012

NADAL NJE WEMBLEDON.

Lukas Rosol

BINGWA mara mbili wa michuano ya Wimbledon Rafael Nadal ameondolewa katika michuano hiyo inayoendelea jijini London baada ya kukubali kipigo cha seti tano kutoka kwa Lukas Rosol ambaye yuko katika nafasi ya 100 katika orodha za ubora wa mchezo huo duniani. Katika mchezo huo Nadal ambaye anashika namba mbili katika orodha hizo alishindwa kutamba kwa Rosol mwenye umri wa miaka 26 raia wa Jamhuri ya Czech kwa 6-7 6-4 6-4 2-6 6-4 katika mzunguko wa pili wa michuano hiyo. Hii ni mara ya kwanza kwa Nadal kutolewa katika mzunguko wa pili wa michuano mikubwa toka alipofungwa na Gilles Mueller katika mzunguko wa pili wa michuano ya Wimbledon mwaka 2005. Matokeo hayo yamemsafishia njia Andy Murray wa Uingereza ambaye ilikuwa akutane na Nadal ambaye ni raia wa Hispania katika hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo.

No comments:

Post a Comment