Friday, June 29, 2012

MBEYA UPDATE: WANAKIJIJI WAMVUA UONGOZI MWENYEKITI

W
ananchi wa Kijiji cha Isyonje,Kata ya Isongole,Wilaya ya Rungwe Mkoani Mbeya wamemvua uongozi,mwenyekiti wa kijiji hicho Venance Daima na halmashauri ya kijiji kizima kwa tuhuma za ubadhilifu wa mali na kutosimamia ipasanyo rasilimali za kijiji ikiwemo mianzi ya asili na mashamba ya kijiji.

Tuhuma hizo zimetolewa katika mkutano maalumu wa kijiji hicho uliofanyika Juni 28 mwaka huu mbele ya Diwani wa kata hiyo Laurence Nyasa Mfwango,ambapo baada ya kupitia taarifa ya mapato na matumizi iliyosomwa na Afisa mtendaji wa kijiji hicho Bwana Ambokile Kinjisi na kubaini kuwa jumla ya shilingi 1,118,000 kufunjwa na mhasibu wa kijiji Bwana Michael Mbilinyi.
 
Aidha mhasibu huyo alipotakiwa kuonyeshwa pesa hizo zilipo alishindwa hali iliyompelekea kukiri kosa hilo na kuahidi kuzilipa Juni 29 mwaka huu baada ya kujiwekea dhamana ya shamba la miti.

Hata hivyo wananchi hao waliutupia lawama uongozi wa kijiji kwa kutosimamia mali ikiwa ni pamoja na uuzaji holela wa mianzi na ukodishwaji wa mashamba bila ridhaa ya wananchio na kutoitisha mikutano ya hadhara ikiwa ni kinyume na kanuni za Serikali ya kijiji.

Katika hali isiyokuwa ya kawaida baada ya tuhuma hizo wananchi walimtaka mwenyekiti huyo na halmashauri yake kujiuzuru,ambapo walikubaliana na kijiji hicho kusimamiwa na kamati ya mpito,chini ya Afisa mtendaji wa kijiji Bwana Kinjisi.

Kutokana na wananchi kuchoshwa na uongozi  huo baadhi yao waliondoka mkutanoni kwa hasira  na viongozi wa kijiji kuacha viti vyao na kumuacha Diwani,ambaye alilazimika kufunga mkutano.baada ya mwenyekiti aliyeufungua mkutano huo na wananchi wakaridhia Kamati ya watu 10 kusimamia shughuli za kimaendeleo hadi uongozi mwingine utakapochaguliwa kwa mujibu wa kanuni za kijiji.
Imeandikwa na Ezekiel Kamanga, Mbeya

No comments:

Post a Comment