Saturday, June 30, 2012

DOS SANTOS KUTIMKIA ATLETICO MADRID.

KIUNGO wa kimataifa wa Mexico na klabu ya Tottenham Hotspurs Giovani dos Santos anatarajiwa kuikacha klabu yake hiyo baada ya kuruhusiwa kuondoka katika kambi ya kikosi cha nchi hiyo kinachojiandaa na michuano ya olimpiki ili aweze kushughulikia uhamisho wake wake. Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 23 ana thamani ya paundi milioni nane ana anatarajiwa kujiunga na klabu ya Atletico Madrid ya nchini Hispania mwishoni mwa wiki hii baada ya kutua London. Nayo klabu ya Paris Saint-Germain imeendelea na mbio zake za kumuwania mshambuliaji wa Manchester City Carlos Tevez mwenye umri wa miaka 28. Mbali na Tevez pia klabu hiyo ambayo imeonyesha nia ya kumwaga fedha nyingi katika kipindi hiki cha usajili pia inamuwania beki wa kimataifa wa Brazil na klabu ya AC Milan, Thiago Silva ambaye ana umri wa miaka 27. Mkurugenzi wa michezo wa klabu hiyo tajiri ametamba kuwa pesa usajili sio tatizo kwa klabu hiyo ila jambo linawapa tatizo ni kuwashawishi wachezaji hao ili waweze kujiunga na klabu hiyo.

No comments:

Post a Comment