Monday, July 2, 2012

TORRES ANYAKUWA KIATU CHA DHAHABU EURO 2012.

MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Hispania, Fernando Torres amenyakuwa kiatu cha dhahabu kama mfungaji bora wa michuano ya Ulaya iliyomalizika jana baada ya kufunga mabao matatu ambayo amefunga katika dakika 189 pekee alizocheza katika michuano hiyo. Torres ambaye alicheza katika kipindi cha pili akitokea benchi la wachezaji wa akiba alifunga bao la tatu katika dakika ya 84 kwenye mchezo ambao timu yake hiyo ilishinda mabao 4-0 dhidi Italia huku mengine mawili akifunga wakati timu hiyo ilipopata ushindi wa mabao 4-0 dhidi Jamhuri ya Ireland katika hatua ya makundi ya michuano hiyo. Wachezaji sita wamemaliza michuano hiyo wakiwa na mabao matatu sawa na Torres katika michuano hiyo lakini mchezaji huyo amepewa tuzo hiyo kutokana na kutoa pasi nyingi zilizozaa mabao tofauti na wengine. Wachezaji wengine waliomaliza wakiwa na mabao matatu katika michuano hiyo ni pamoja na Mario Balotelli-Italia, Alan Dzagoey-Urusi, Mario Gomez-Ujerumani, Mario Mandzukic-Croatia, Cristiano Ronaldo-Ureno.

No comments:

Post a Comment