Tuesday, July 3, 2012

WASIFU 360: PEPE KALLE

Pepe Kallé (Novemba 30, 1951 - 28 Novemba, 1998) alikuwa mwimbaji wa soukous, mwanamuziki na kiongozi wa bendi kutoka nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Pepe Kallé alipozaliwa alipewa jina Kabasele Yampanya katika mji mkuu wa Kinshasa(wakati huo mji huu ulikuwa unajulikana kama Léopoldville), lakini baadaye aliamua kulichukua jina la mshauri wake, Grand Pepe Kalle.

Pepe Kalle alikuwa na uwezo wa kuimba kwa sauti ya juu zaidi pamoja na sauti ya chini zaidi ambayo kwa lugha ya kimombo inaitwa “multi-Octave range”. Pepe Kalle alikuwa akiingia jukwani anatambulika mara moja kwani alikuwa na urefu wa sentimita 190 (fiti 6 inchi 3) na uzito wa kilogramu 136 (puandi 300). Mwimbaji huyu alirekodi zaidi ya nyimbo mia tatu na Albamu ishirini katika wasifu wake wa miongo miwili mirefu ya muziki. Kwa wapenzi wake wa muziki alikuwa anajulikana kama "tembo wa muziki Halisi ya Afrika " na "La Bombe Atomique" kwani Pepe Kalle aliwatumbuiza watazamaji tendaji zake za nguvu.

Wasifu wake wa kimuziki ulianza na African Jazz, bendi ya Grand Pepe Kalle. Baadaye akawa mwimbaji kiongozi wa Lipua Lipua, ambapo aliimba sambamba na Nyboma Mwandido. Mwaka wa 1972, Pepe Kalle pamoja na Dilu Dilumona na Papy Tex, waliiacha bendi ya Lipua Lipua na kuunda bendi yao wenyewe iliyokuwa ikiitwa Empire Bakuba. Empire Bakuba ilichukua jina lake kutoka kabila ya kishujaa ya Kikongo, na kundi hili lilingiza ngoma na midundo ya muziki kutoka ndanindani, sauti ambazo zilikuwa zimetupiliwa mbali kwa muda mrefu na rumba maarufu. Bendi hii ilikuwa maarufu mara moja na pamoja na Zaiko Langa Langa wakawa bendi za vijana maarufu zaidi katika mji mkuu wa Kinshasa. Pamoja na vibao motomoto kama Dadouya Pepe Kallé na Sango ya mawa ya Papy Tex, bendi hii daima ilishirikishwa kwenye chati ya muziki. Wao pia waliumba njia mpya ya kucheza au kusakata iliyojulikana kama kwassa kwassa.

Katika mwaka wao wa kumi tangu kuanzishwa kwao mwaka wa 1982, bendi hii iliteuliwa kama kundi cha juu zaidi nchini Zaire. Katika miaka ya mapema ya 1980, Empire Bakuba iliendelea ziara zake za mbali huku ikitoa zaidi ya albamu nne kwa mwaka. Katikati ya miaka za 1980, walikuwa na wafuasi wengi katika Kati ya Francophone na Afrika Magharibi. Ushirikiano wake wa mwaka wa 1986 pamoja na Nyboma iliyokuwa ikiitwa Zouke Zouke ilikuwa mmoja kati ya Albamu zilizouzwa sana mwaka huo. Lakini ilikuwa ushirikiano wake wa pili na Nyboma, Moyibi (mwaka wa 1988), ambayo ilianzisha umaarufu wake kote Afrika.
Mwishoni mwa miaka ya 1980 na mapema miaka ya 1990, Pepe Kalle aliunganisha vipengele vya soukous vilivyochezwa kwa kasi ambavyo viliundwa katika studio za Paris. Albamu yake ya mwaka wa 1990, Roger Milla, iliyotoa shukrani kwa talanta na ujuzi wa mwanakandanda huyu mkuu kutoka Kamerun, ni mfano maridadi wa mpangilio huu.

Mwaka wa 1992, bendi ilikabiliwa na msiba wake wa kwanza mkubwa wakati Emoro, mbilikimo wa kusakata rhumba wa bendi, aliupa dunia mkono wa buriani wakati walikuwa ziarani nchini Botswana. Licha ya msiba huu, umaarufu wa Pepe Kallé uliendelea kuenea katika miaka ya tisini kwani alitoa Albamu kama Gigantafrique, Larger than life na Cocktail . Alishirikiana na wanamuziki wa kitambo mashuhuri kama vilevile Lutumba Simaro na Nyoka Longo.

Pepe Kallé aliaga dunia kutokana na mshtuko wa moyo mnamo Novemba 1998.

No comments:

Post a Comment