Thursday, July 5, 2012

MBEYA UPDATE: AFARIKI KWA KUTUMBUKIA KATIKA SHIMO LA MAJI MACHAFU


Mtoto mmoja aitwaye Bonifance  Edward mkazi wa kijiji cha Ilolo  jijinj Mbeya amefariki dunia baada ya kutumbukia kwenye shimo la maji machafu wakati akicheza na watoto wenzake.

Kamanda wa polisi mkoani Mbeya Bw.Diwani  amesema tukio hilo limetokea julai 3 mwaka huu majira ya saa nane mchana katika eneo la Ilolo jijini hapa.

Diwani amesema kuwa mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali ya Rufaa mkoani Mbeya.

Katika hatua nyingine  Bw Athumani amewataka wazazi na walezi kuhakikisha mazingira yanayo wazunguka watoto na jamii kwa ujumla kuwa salama ili kuepukana na matatizo kama hayo.

No comments:

Post a Comment