Wednesday, July 4, 2012

TUJIKUMBUSHE: JAVIER MARTINEZ WA ATLECTICO MADRID ATIMULIWA KUPIGA PICHA SIKU HISPANIA ILIPOCHUKUA KOMBE LA EURO 2012

Wakati Spain walipokuwa wamekabidhiwa kombe lao la Euro wachezaji wa Barcelona na Real Madrid walianza kuchukua kombe na kuanza kupiga nalo picha kwa kila kundi la wachezaji wa timu hizo mbili kupiga picha ya pamoja na kombe.


Walianza Barceona ambao wao ndio wengi kwenye kikosi cha Spain wakapiga picha na kombe kisha wakawabidhi wa Real Madrid - wakiongozwa na nahodha Iker Casillas, Raul Albiol, Arbeloa, Xabi Alonso na Sergio Ramos walijipanga kupiga picha na kombe na ghafla akaibuka Javier Martinez wa Atletico Madrid na kujipanga nao - kwa utani mchezaji mwingine akisaidiana na Sergio Ramos wakamtoa kwenye sehemu ya kupiga picha hiyo maalum kwa wachezaji wanaochezea Madrid.

No comments:

Post a Comment