Wednesday, July 4, 2012

TANZANIA FOOTBALL NEWS: SIMBA YAIKUNG'UTA MAFUNZO 2-1

Siku moja baada ya kutoka sare na klabu ya Express ya Uganda, mabingwa wa Tanzania bara klabu ya Simba imeanza vyema michuano ya kombe la Urafiki huko Zanzibar baada ya kuwagonga wala urojo klabu ya Mafunzo   kwa mabao mawili kwa moja.

Alikuwa ni kinda jipya la klabu hiyo lilosajiliwa kutoka klabu ya Ruvu Shooting aliyefunga mabao ote mawili katika dakika ya 27 na 44, huku pasi za mwisho zote zikitolewa na kiungo mpya wa timu hiyo Kanu Mbivayanga raia wa DRC Congo.

Kwenye dakika ya 80 Mafunzo walikuja juu na kufanikiwa kufunga bao la kufutia machozi  lililofungwa Jaku Joma

Timu zilianza hivi
Simba; Juma Kaseja, Haruna Shamte, Amir Maftah/Paul Ngalema, Lino Masombo, Shomary Kapombe, Amri Kiemba, Danny Mrwanda/Mwinyi Kazimoto, Mussa Mudde/Paul Ngalema, Abdallah Juma/Uhuru Suleiman, Kanu Mbivayanga/Haroun Othman na Kiggi Makassy.

Mafunzo: Suleiman Janabi, Hajji Abdi, Ally Juma, Yussuf Makame, Said Mussa, Juma Othman, Abdulrahim Mohamed, Suleiman Kassim ‘Selembe’, Ismail Khamis, Juma Jaku na Ally Othman.

No comments:

Post a Comment