Thursday, July 5, 2012

HISPANIA HAIJAFIKIA UBORA WA KIKOSI CHA BRAZIL MWAKA 1970 - PELE.

Pele.

MCHEZAJI nyota wa zamani wa Brazil, Pele amesema kuwa kikosi cha nchi hiyo ambacho kilinyakuwa Kombe la Dunia mwaka 1970 kilikuwa na wachezaji wengi wenye vipaji ukilinganisha na kikosi cha sasa cha Hispania ambacho kimefanikiwa kutetea taji la michuano ya Ulaya. Akiulizwa kuwa ni timu ingeshinda kati ya hiyo ya Brazil ya mwaka 1970 na Hispania ya hivi sasa nyota huyo wa zamani alijibu kwa kujiamini kwamba kama angekuwa anacheza isingekuwa na shaka kwamba wangeshinda mtanange huo. Hispania ambao wameshinda mataji mawili ya Ulaya mfululizo pamoja na lile la Kombe la Dunia 2010 imekuwa timu ya kwanza katika historia kushinda mataji matatu makubwa ya kimataifa. Ustadi wa kumiliki mpira ulioonyshwa na wachezaji wa Hispania na kuwasadia kutete taji lao hilo umefananishwa na ule wa kikosi cha Brazil cha mwaka 1970 ambacho kilikuwa na wachezaji kama Pele, Rivellino, Gerson, Tostao na Jairzinho ambao walinyakuwa Kombe la Dunia nchini Mexico kwa kuifunga Italia kwa mabao 4-1 katika mchezo wa fainali. Pele alistaafu kucheza soka mwaka 1971 na hakuwepo katika kikosi cha Brazil ambacho kilishiriki michuano ya Kombe la Dunia mwaka 1974 ambapo kilimaliza katika nafasi ya nne.

No comments:

Post a Comment