Sunday, July 1, 2012

SEEDORF ATIMKIA BRAZIL.

Clarence Seedorf.

KLABU ya Botafogo ya nchini Brazil imekubali kumsajili kiungo wa kimataifa wa Uholanzi Clarence Seedorf ambaye ana umri wa miaka 36 kwa mkataba wa miaka miwili. Rais wa klabu hiyo Mauricio Assuncao alithibitisha ujio wa mchezaji huyo katika klabu hiyo baada ya taarifa kutoka katika mtandao wa klabu hiyo juu ya ujio wake. Assuncao amesema kuwa Seedorf haji nchini humo kwa ajili ya kufuata pesa bali ni changamoto katika soka la Brazil ndiyo zilizomfanya aje amalizie soka lake nchini humo hivyo hatua klabuni hapo kwa ajili ya matembezi. Seedorf ambaye mkataba wake na klabu ya AC Milan ya Italia ulimalizika mapema mwezi huu baada ya kuitumikia klabu hiyo kwa miaka 10, ameoa mwanamke wa kibrazil na mara kwa mara ameonekana akiwa katika mapumziko katika fukwe za jiji la Rio de Janeiro. Kiungo huyo ameshinda mataji mawili kati ya manne ya michuano ya Klabu ya Ulaya akiwa na Milan ambapo ni mmoja wa wachezaji wenye umri mkubwa katika klabu hiyo ambao wameondoka msimu wa majira ya kiangazi.

No comments:

Post a Comment