Sunday, July 1, 2012

NYOTA WA NBA AENGULIWA KIKOSI CHA UINGEREZA.

Ben Gordon.

NYOTA wa mpira wa kikapu wa anayecheza katika Ligi Kuu ya mchezo huo nchini Marekani-NBA Ben Gordon ameenguliwa katika kikosi cha timu ya taifa ya Uingereza baada ya kushindwa kuripoti katika kambi ya timu hiyo katika tarehe ya mwisho ambayo ilikuwa Juni 30 mwaka huu. Gordon ambaye anacheza katika klabu ya Charlotte Bobcats nafasi ya ulinzi alitajwa katika orodha ya wachezaji ambao watachujwa Aprili mwaka huu na kocha mkuu wa timu hiyo Chris Finch ambaye alikuwa akitegemea kumjumuisha katika kikosi chake cha mwisho. Kushindikana kutokea katika kambi hiyo kwa nyota huyo kumesababisha kikosi hicho kupwaya katika sehemu ya ulinzi na kupelekea kushindwa katika michezo yao mitano ya kujipima nguvu ambayo wamecheza wakiwa katika kambi waliyoweka huko Texas, Marekani. Gordon ambaye amejiunga na Bobcats akitokea timu ya Detroit Pistons mapema wiki hii amekuwa akijumuishwa katika kikosi cha Uingereza toka mwaka 2008 lakini hajawahi kucheza hata mchezo mmoja kutokana na majeruhi, matatizo ya kifamilia pamoja na majukumu mengine. Kikosi hicho kinatarajiwa kurejea nchini uingereza baada ya kushindwa mechi zake zote walizocheza nchini Marekani ukiwemo mchezo mmoja waliocheza na Nigeria na miwili katika kila timu za Lithuania na Urusi.

No comments:

Post a Comment