K |
ushamiri kwa mfumo dume katika wilaya ya Mbeya kunaathiri kwa kiasi kikubwa hali ya kiuchumi kwa wanawake ambao ndio nguvu kazi kubwa katika kilimo, kipato wanmachopata baada ya mavuno huishia mikononi mwa wanaume wanaojihusiusha na vitendo vya starehe na kusahau malezi ya familia zao.
Uchunguzi umebaini kuwepo kwa vitendo vya unyanyasaji na ukatili wanavyofanyiwa wanawake wa vijiji vya Ifiga,Iwalanje na Nsongwi juu Kata ya Ijombe vinavyotokana na nguvu ya wanaume ya kuhodhi mali zilizopatikana kwa kuwashirikisha wanawake.
Mmoja wa wanawake wa Kijiji cha Ifiga Bi Salah Jailos alisema kuwa wakati wa msimu wa kilimo unapowadia hushirikiana na waume zao kwa karibu bila kuwepo ugomvi wowote ndani ya familia zao mpaka mazao yanapokomaa.
Alisema kuwa inapofika kipindi cha kuvuna wanaume huanza kubadilika kwa kutafuta sababu mbali mbali za kuonyesha chuki ndani ya nyumba ili aweze kupata sababu za kuvuna peke yake mazao na kuuza pepe yake bila kumshirikisha mke wake.
Mwanamke mwingine mkazi wa Usongwe Juu Bi.Benadeta Hamisi alisema kufutia vitendo hivyo vya wanaume tunaomba waache kwani iweje wakati wa kilimo tulime wote lakini inapofika wakati wa mavuno wawe wababe wa kuuza mazao9 peke yao kwa ujumla huu ni ukatili wa kijinsia kwa sisi wanawake wa Kata ya Ijombe.
Hata hivyo mwanamke huyo alisema athari ambazo wanapata baada ya kuachiwa familia ni kupata shida ya kuhudumia familia ikiwa ni pamoja na kusomesha watoto namahitaji mengine ya nyumbani ambayo ni muhimu.
Akizungumzia malalamiko hayo kwa Wanawake wa vijiji hivyo, Mwenyekiti wa serikali ya kijiji cha Ifiga Bw.Raphael Siyejele alisema hana taarifa za kiofisi za wanaume kuwanyanyasa wake zao labda kama zipo ngazi zingine.
Uchunguzi umebaini kuwepo kwa vitendo vya unyanyasaji na ukatili wanavyofanyiwa wanawake wa vijiji vya Ifiga,Iwalanje na Nsongwi juu Kata ya Ijombe vinavyotokana na nguvu ya wanaume ya kuhodhi mali zilizopatikana kwa kuwashirikisha wanawake.
Mmoja wa wanawake wa Kijiji cha Ifiga Bi Salah Jailos alisema kuwa wakati wa msimu wa kilimo unapowadia hushirikiana na waume zao kwa karibu bila kuwepo ugomvi wowote ndani ya familia zao mpaka mazao yanapokomaa.
Alisema kuwa inapofika kipindi cha kuvuna wanaume huanza kubadilika kwa kutafuta sababu mbali mbali za kuonyesha chuki ndani ya nyumba ili aweze kupata sababu za kuvuna peke yake mazao na kuuza pepe yake bila kumshirikisha mke wake.
Mwanamke mwingine mkazi wa Usongwe Juu Bi.Benadeta Hamisi alisema kufutia vitendo hivyo vya wanaume tunaomba waache kwani iweje wakati wa kilimo tulime wote lakini inapofika wakati wa mavuno wawe wababe wa kuuza mazao9 peke yao kwa ujumla huu ni ukatili wa kijinsia kwa sisi wanawake wa Kata ya Ijombe.
Hata hivyo mwanamke huyo alisema athari ambazo wanapata baada ya kuachiwa familia ni kupata shida ya kuhudumia familia ikiwa ni pamoja na kusomesha watoto namahitaji mengine ya nyumbani ambayo ni muhimu.
Akizungumzia malalamiko hayo kwa Wanawake wa vijiji hivyo, Mwenyekiti wa serikali ya kijiji cha Ifiga Bw.Raphael Siyejele alisema hana taarifa za kiofisi za wanaume kuwanyanyasa wake zao labda kama zipo ngazi zingine.
No comments:
Post a Comment