Thursday, June 21, 2012

TANZANIA BOXING NEWS: LORENZ AWASILI KILIMANJARO


Mcheza sinema toka Marekani Deidre Lorenz amewasili mjini Moshi tayari kushiriki kwenye mbio za Mt. Kilimanjaro Marathon zitakazofanyika juni 24. Lorenz amwasili leo na ndege ya Ethiopian Airlines ambao ndio wafadhali wa mbio za Mt. Kilimanjaro Marathon zinazofanyika jumapili ya mwisho ya mwezi wa sita kila mwaka.

Ujio wa Lorenz ambaye amecheza sinema nyingi zikiwamo Santorini Bule, Perfect Strangers, The Big Fight umeleta msisimko mkubwa katika mji huu mkuu wa Kilimanjaro. Ujio wake umefuatia matayarisho ya muda mrefu ambayo yanaendana na hadhi yake. 

Akizungumza na waandishi wa habari waliofika kumshuhudia mcheza sinema huyu, Lorenz alisema kuwa ameisikia kuwa mlima wa Kilimanjaro uko Kenya kwa kwa muda mrefu na ana furaha kubwa sana ya kufika ili kushughudia kuwa mlima huu maarufu duniani uko Tanzania. “Nimekuwa nautangaza sana ujio wangu kwenye blog na tovuti yangu, wapenzi wangu pamoja na watu wengi wanangojea kurudi kwangu nikawaambie niliyoyashughudia” alisema Deidre Lorenz ambaye ameshawahi kuteuliwa zaidi ya mara tatu kwa tuzo za Oscar. Lorenz alisema kuwa kwa miaka mingi alifikiri kuwa mlima Kiliamnjaro uko Kenya kwa jinsi nchi hiyo jiraniminavyoutangaza nchini Marekani.

“Sasa nimeona mwenyewe kwa macho yangu kuwa kweli mlima (Kilimanjaro) huu maarufu duniani uko Tanzania na sio Kenya” alisema Deidre Lorenz ambaye anaishi kwenye jiji la New York City linalofahamika kama jiji la pesa (International Financial Capital) la kimataifa. Lorenz ameshukia katika hoteli ya Bristol Cottages iliyopo karibu na benki ya Standard Chattered mkabala na bustani ya Manispaa ya Uhuru Park.
 Mji wa Moshi na viunga vyake vinarindima kwa ujio wa watalii wengi kutoka Marekani ambao wamekuja kushiriki kwenye mbio hizi zilizojijengea umaarufu mkubwa kwa kuitangaza Tanzania nchini Marekani. Mbio za Mt. Kilimanjaro Marathon zilianzishwa na Marie Frances mwaka 1991 baada ya kuombwa na balozi wa zamania wa Tanzania nchini Misri.
Mbio hizi zimejijengea umaarufu mkubwa na zimeshawahi kupata tuzo nyingi baadhi zikiwa zimetolewa na Wonders of the World Magazine lenye wasomaji zaidi ya milioni 5 likiwa limezipa nafasi ya 2 kama mbio zenye hadhi ya kukimbiwa duniani wakati jarida la Forbes la Marekani  lenye wasomaji wengi duniani limeipa nafasi ya kwanza. Ndio maana Manispaa ya Moshi itampa barabara na kuiita “Marie Frances Boulevard”mwaka 2009.
Mbio hizi hukimbiwa na watalii wa Warekani wanaokuja Tanzania kupanda mlima Kilimanjaro na kutembelea mbuga za wanyama. Mt. Kilimanjaro Marathon zinajulikana kama 7 continental races zikiwa zinakimbiwa katika mabara 7 ya dunia.
Ratiba ya Deidre Lorenz inaonyesha kuwa kesho ijumaa atakitemnbelea kituo cha watoto yatima cha Upendo kinachoendeshwa na watawa wa Precious Blood. Lorenz atakaa na watoto hao na kuwasomea hadithi mbalimbali za watoto zilizoandikwa na Waltz Disney mwandishi maarufu wa karne ya ishirini wa Marekani.
Siku ya jumamosi atatembelea hospitali ya KCMC ambapo atakutana na manesi ili kuwapa shavu kwa kazi yao nzuri wanayoifanyia jamii. Jioni ya jumamosi atahudhuria Pasta Party ambapo atapata nafasi ya kukutana na wakimbiaji wengine na kuchagua namba ya kukimbia kesho yake siku ya jumapili tarehe 24 juni.
Imetumwa na:
Grace Soka
Afisa Uhusiano

No comments:

Post a Comment