Thursday, June 21, 2012

MBEYA UPDATE: WAHABESHI 2 WAKAMATWA


Watu watatu wenye asili ya Ethiopia wamekamatwa na Maafisa wa Jeshi la Polisi mkoani Mbeya kuwa kuingia nchini bila kibali.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Jeshi hilo imesema wahabeshi hao walikamatwa majira ya saa 1 jioni juzi  maeneo ya  Uyole Jijini Mbeya.

Taarifa hiyo imewataja waliokamatwa kuwa ni  Murugeta Dejene (28), Masele Fuge (22) na Kakere Tadeos (25)  na kuongeza kuwa wahabeshi wengi wanaokamatwa nchini ni wale wanaokimbia ukame na njaa pia vita.

Aidha taarifa hiyo imesema watuhumiwa wapo mahabusu wakisubiri taratibu za kukabidhiwa Idara ya Uhamiaji kwa hatua zaidi.

No comments:

Post a Comment