S |
emina Elekezi ya siku moja kwa Wratibu na Waandishi wa Habari kuhusu mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Kanda Nyanda za Juu Kusini inaendelea katika Ukumbi wa Mikutano wa Hospitali ya Mkoa wa Mbeya.
Katika Semina hiyo Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mkoa wa Mbeya Dk. Seif Mhina akifungua amewataka wadau wa semina hiyo kushiriki kikamilifu katika kutoa michango yao kwa manufaa ya watumiaji nchini.
Mada husika ni
· Mpango wa Kina Mama Wajawazito wasio na uwezo (KFW).
· Ujazaji wa Fomu za Madai, Madai ya kughushi, bei Mpya za Huduma zitolewazo.
Katika Semina elekezi hiyo Meneja wa Kanda ya Nyanda za Juu Kusini Celestin Muganga amehudhuria.
No comments:
Post a Comment