Friday, June 22, 2012

MBEYA UPDATE: AUAWA NA WANANCHI WENYE HASIRA KALI


M
arehemu Mwile akiwa na mtuhumiwa mwenzake Bwana Frank Nzovu(Tembo) ambaye alitokomea kusikojulikana na ni mwenyeji wa Kijiji cha Ikonya,Wilaya ya Mbozi,walifika nyumbani kwa Bwana Shigela ambapo waliwachukua wafanyabiashara hao hadi eneo la shamba walikodai kuwepo kwa ufuta.
Baada ya kufika eneo hilo hali ilikuwa ndovyo sivyo baada ya vijana hao kugeukia wafanyabiashara hao na kuwatishia mapanga wakidai wapewe pesa,ambapo Bwana Mwalindu alitoa pesa taslimu shilingi 860,000 na Bi.Mpamba alitoa shilingi 700,000 baada ya kukatwa kiganja cha mkono wa kushoto na wahalifu kutokomea kusikojulikana.

Kufuatia tukio hilo majeruhi walitoa taarifa katika Afisa Mtendaji wa kijiji Bwana Bahati Mwanguku na Mwenyekiti Bwana Nestory Mwashadema,ambao nao walitoa taarifa katika Kituo cha Polisi cha Galula na walifika eneo la tukio na kuwa tafuta watuhumiwa bila mafanikio.

Polisi walirudi siku ya pili kwa ajili ya kukitafuta kiganja cha mkono cha Bi Mpamba ambapo walifanikiwa kukikuta na majeruhi kukiwakilisha kituoni hapo na kukimbizwa katika Hospitali teule ya Ifisi May 26 mwaka huu,siku moja baada ya tukio hilo majira ya saa sita mchana.

Kwa upande wake Afisa Mtendaji wa kijiji hicho Bwana Mwanguku,amewataja watuhumiwa wanaodaiwa kumkata kiganja mwanamke huyo kuwa ni pamoja na Karim(anayedaiwa kushika kisu),Frank Nzovu(alishika panga),Shigela na Mwile Hassan.

Watuhumiwa hao baada ya kutoroka ndipo wananchi walianza msako mkali na kufanikiwa kumkamata Shigela na Mwile Hassan,ambaye alikamatwa Juni 21 mwaka huu usiku akiwa amejificha kichakani baada ya kutoroka kwa baba yake Bwana Hassan Mwahasanga(60) kilometa 8 kutoka eneo la tukio kijiji cha Masalamba,Chunya.

Katika mapambano wananchi wenye hasira kali walimkamata mtuhumiwa hadi Ofisi ya kijiji na baada ya kupishana na Afisa Mtendaji wa kijiji,waliamua kuchukua matita ya ufuta na petroli ndipo walipoamua kuwasha moto na kumteketeza mtuhumiwa ambapo kifua ba kichwa ndivyo vilisalia.

Polisi walifika eneo la tukio saa moja baada ya tukio kufanyika majira ya saa 5 asubuhi na kuufanyia uchunguzi mwili wa marehemu na mara baada ya kukamilika ndugu wa marehemu walikabidhiwa kwa ajili ya masomo.

Baba wa mtuhumiwa Bwna Hassan Mwahasanga,amethibitisha kuwa mwanae ndiye aliyeuawa ingawa ameeleza kuwa hajui chanzo cha tukio.

Aidha wananchi wa kijiji hicho,ambao hawakupenda majina yao kutajwa,wamesema wamechoshwa na tabia za vijana wa hao kijijini hapo na wao wameamua kufanya hivyo ili iwe onyo kwa vijana wengine kujihusisha na vitendo vya uporaji.

Mazishi ya marehemu yamefanyika katika Kijiji cha Totowe Juni 22 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment