Thursday, June 14, 2012

GLOBAL NEWS: AFRIKA INAWEZEKANA KUONDOKANA NA BAA LA NJAA


Wakati Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara ikiendelea kukabiliwa na baa la njaa na upungufu mkubwa wa chakula. Taarifa zinaonyesha kwamba Afrika inaweza kabisa kuondokana na hali hiyo pale tu viongozi wake watakapoonyesha utashi wa kisiasa na dhamira ya dhati ya kujinasua na baa hilo.
Ameyasema hayo wakati wa uwasilishaji wa ripoti ya mwaka 2012 ya maendeleo ya Binadamu Afrika, ripoti ambayo iliwasilishwa kwa Mabalozi wa Afrika wanaoziwakilisha nchi zao katika Umoja wa Mataifa.

Migiro anasisitiza kama ambavyo viongozi wa Afrika wamekuwa wakishirikiana katika kuzikabili changamoto nyingine, wanaweza pia kushirikiana katika kukuza kilimo na uzalishaji wa chakula na hatimaye kuwa na usalama wa chakula ambao ni wakudumu.

Ripoti hiyo ambayo maudhui yake ni “ kuelekea usalama wa chakula”imetayarishwa na Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa, ( UNDP) kanda ya Afrika, na ni mahususi kwaajili ya Afrika kusini mwa Jangwa la Sahara.

Ni ripoti ambayo imeelezea kwa nini Afrika imeendelea kuwa ombaomba wa chakula, ikianisha pia na kutoa mapendekezo yakiwamo kama ya uendelezaji wa miundombinu ya vijijini, uwezeshaji wa wakulima wadogo wakiwamo wanawake, uwekezaji katika kilimo na pembejezo za kilimo, uhakika wa chakula hicho kufika mezani na lishe bora.

Akizungumzia ripoti hiyo, ambayo anasema tayari imeibua mijadala katika vyombo vya habari. Migiro anasema ripoti imekuja wakati muafaka ambapo Jimbo la Sahel ya Magharibi likiwa katika shida kubwa ya chakula huku watu milioni 13 wakiwa katika hatari kubwa ikiwa ni pamoja na watoto milioni moja.

Akasema inatia moyo kwamba viongozi wa Afrika wameanza kuchukua hatua mbalimbali za kulikabili janga hilo. Lakini inatia moyo zaidi pale ambapo viongozi wa mataifa tajiri akiwamo Rais Barack Obama wanapojitokeza na kuelezea nia yao ya kusaidia ukuaji wa sekta ya kilimo katika afrika na kuwaondoa watu milioni 50 kutoka katika umaskini katika kipindi cha miaka 10 ijayo.

Amebainisha viongozi hao wa mataifa tajiri zaidi duniani (G8) wamereja tena kauli yao waliyoitoa huko L’ Aquila, ahadi ya kuongeza misaada ya kifedha inayolenga kusaidia mipango ya kitaifa.

Aidha anasema anaimani kwamba ikiwa mpango wa mapinduzi ya kijani ambao umeandaliwa mahususi kwaajili ya Afrika, mpango ambao yeyé aliusimamia kuwa, kama ukitekelezwa vizuri utatoa mchango mkubwa kwa kuwa na usalama wa chakula.

Kwa upande wake, BW. Tegegnework Gettu ambaye ni Naibu Katibu Mkuu na Mkurugenzi wa UNDP kanda ya Afrika, yeyé alisema Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara haina sababu ya kuendelea kuwa na uhaba mkubwa wa chakula kutokana kwamba ina hazina kubwa ya ardhí inayofaa kwa kilimo, mito na maziwa ya kutosha na raslimali watu.

Akabainisha kwamba haiingi katika fikra kwamba ni kwanini licha ya Uchumi wa Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara kuonyesha ukuaji mzuri lakini suala la usalama wa chakula limeendelea kubaki tatizo kubwa.

Akahoji pia kwamba kama nchi za India na Amerika ya Latini ziliweza kuondokana na uhaba wa chakula kwa kutumia mapinduzi ya kijani,( Green Revolution) kwanini hali inakuwa tofauti kwa Afrika kusini mwa Jangwa la Sahara.

No comments:

Post a Comment