Saturday, April 28, 2012

FIFA TO TEST GOAL-LINE TEKNOLOGY IN LIVE MATCHES.

SHIRIKISHO la Soka la Dunia-FIFA limepanga kufanya majaribio ya teknologia ya kompyuta katika mstari wa goli katika baadhi ya mechi. FIFA imesema kuwa mfumo unaoitwa GoalRef unatarajiwa kufanyiwa majaribio katika mechi mbili kwenye Ligi Kuu nchini Denmark au watafanya mchezo mmoja kwenye ligi na mwingine kwenye mchezo wa kimataifa wa kifariki. Mfumo mwingine ambao umependekezwa na Bodi ya Kimataifa ya Vyama vya Soka-IFBA ambacho ndicho chombo kinachotunga sheria za mpira, unaitwa Hawk-Eye wenyewe unatarajiwa kufanyiwa majaribio nchini Uingereza Mei 16 mwaka huu katika mchezo wa fainali ya Kombe la FA. IFBA inajipanga kutoa maamuzi yake kama wataruhusu mfumo huo utumike katika mkutano wao unaotarajiwa kufanyika Julai 2 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment