Wednesday, April 25, 2012

CITY KUFANYA ZIARA MALAYSIA.

KLABU ya Manchester City inatarajiwa kucheza mchezo wa kirafiki na nyota wa Malaysia mchezo ambao utafanyika jijini Kuala Lumpur Julai mwaka huu. City itakuwa katika ziara nchini humo wakati watakapocheza mchezo huo katika Uwanja wa Bukit Jalil ambao una uwezo wa kuchukua mashabiki 90,000 Julai 30 mwaka huu. Makamu wa rais wa Chama cha Soka cha Malaysia, Tengku Abdullah Sultan Ahmad Shah alithibisha kuwepo kwa mchezo huo na kusema kuwa ni heshima kubwa kwao kuwa nchi pekee barani Asia kucheza na City katika ziara yao ya kwanza barani humo. Mabingwa hao wa Kombe la Chama cha Soka cha Uingereza-FA pia watacheza na Arsenal katika Uwanja wa Bird Nest jijini Beijing, China Julai 27 siku ambayo ambayo kutafanyika sherehe za ufunguzi za Olimpiki.

No comments:

Post a Comment