Wednesday, February 22, 2012

Je wajua?....Urusi wanasherehekea Men's Day leo Tar 23 feb

Tarehe 23.02 kila mwaka Warusi husherehekea sikukuu ya wanaume na watu hawaendi makazini wala shuleni kwa maana ni sikukuu kubwa ya Kitaifa. Sikukuu hii ni maalumu kwa kuwakumbuka wanaume wote waliopigana vita kuitetea nchi yao hasa vita ya pili vya Dunia ambapo wanaume wengi walipoteza maisha  kuitetea nchi yao dhidi ya Adolf Hitler aliyeivamia Urusi mwaka 1941 by then ikiitwa USSR. 
 Siku kama ya leo wanaume hua wanapewa zawadi mbalimbali, maua, kuimbiwa  nk (yaani kiujumla leo ni siku yao ya kudeka na kupewa full attention na kua treated like Kings)

   
   Leo wanawake wanaumiza vichwa kujua nini cha kununua au wafanye vipi kufanikisha sherehe hii. Happy Men's day to all Men living in Russia, and all over the world. 

No comments:

Post a Comment