Friday, June 1, 2012

LAMPARD AONDOLEWA TIMU YA TAIFA.



KIUNGO wa kimataifa wa Uingereza na klabu ya Chelsea, Frank Lampard ameondolewa katika kikosi cha timu ya taifa ya nchi hiyo kitakachoshiriki michuano ya Ulaya kutokana na kupata majeraha wakati wa mazoezi ya timu hiyo. Habari ya kuondolewa kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 33 zilitangazwa baada ya madaktari wa timu hiyo kumfanyia vipimo na kugundua kuwa hataweza kupona katika muda wa wiki moja iliyobakia kabla ya michuano hiyo. Kiungo wa klabu ya Liverpool, Jordan Henderson ndio anatarajiwa kuitwa katika kikosi hicho kuja kuziba pengo la Lampard. Akihojiwa kuhusiana na taarifa hizo kocha wa Uingereza Roy Hodgson amesema kuwa ni pigo kubwa kumpoteza mchezaji huyo haswa baada ya kumkosa mchezaji mwingine mzoefu Gareth Barry mapema wiki iliyopita. Hodgson aliendelea kusema kuwa ukweli kwamba madaktari hawawezi kuhakikisha kuwa Lampard hawezi kucheza mchezo wowote katika hatua ya makundi inamaanisha kuwa hawana jinsi zaidi ya kutafuta mbadala wake katika sehemu ya kiungo. Kama Henderson ambaye ana miaka 21 akikubaliwa kuziba nafasi ya Lampard, Liverpool itakuwa ni klabu ambayo ina wachezaji wengi zaidi walioitwa timu ya taifa ya nchi hiyo wakiwa wachezaji watano pamoja na kuwa na msimu mbaya katika Ligi Kuu nchini humo.

Bert van Marwijk: "Afellay can be the Dutch Zidane"


The Netherlands coach has no hesitation to say that Ibrahim Afellay can fulfill the attacking role of the Dutch, which is similar to Zinedine Zidane's preferred position. In the few matches in which he was utilised by Barcelona Afellay has always been played on the wings. The battle for the trequartista position in the Dutch team however, is a tough one, with Welsey Sneijder and Rafael van der Vaart also wanting to fill in that position. van Marwijk is likely to put Afellay on the wings, but with the chance to cut inside in every opportunity. The Oranje manager has said that Zidane played similar to this, because he always cut in from the left.