MBUNGE wa Jimbo la Bahi (CCM), Omary Ahmed Badwel (43) leo amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam,na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa(Takukuru), kwa makosa ya kupokea rushwa ya shilingi milioni moja kutoka kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga, Jonathan Liana.
Wakili wa Takukuru, Janeth Machullia na Ben Lincoln walidai mbele ya Hakimu Mkazi Faisal Kahamba kuwa mshitakiwa huyo anakabiliwa na makosa mawili ya rushwa.
Wakili Machullia alidai kuwa, shitaka la pili ni kwamba kati ya Juni 2 mwaka huu, katika Hoteli ya Peacock, mshitakiwa akiwa na nyadhifa zake zote hizo alipokea rushwa ya milioni moja kutoka kwa Liana ili aweze kwenda kuwashawishi wajumbe wa Kamati hiyo ili waweze kuipitisha ripoti ya fedha ya Halmashauri ya Mkuranga huku akijua kufanya hivyo ni kosa.
Hata hivyo mshitakiwa huyo anayetetewa na wakili wa kujitegemea Mpare Mpoki alikanusha mashitaka yote na wakili wa Machullia alidai kuwa upelelezi wa shauri hilo umekamilika.
No comments:
Post a Comment