Tuesday, June 5, 2012

MBEYA UPDATE: WALIOKUFA KATIKA AJALI YA INTANGANO WAFIKIA 13


Idadi ya waliokufa katika ajali ya jana mchana eneo la Ntangano Ijombe Igawilo Jijini Mbeya imeongezeka na kufikia 13.

Ajali hiyo iliyahusianisha magari mawili Lori lilikuwa likitokea nchini Malawi T658 ASN kuacha njia na kuliparamia basi la Abiria aina ya Coaster lililokuwa lilikitokea Mbeya kwenda Kyela T 188 AWE baada ya mfumo wa breki kushindwa kufanya kazi.

Watu 9 walikufa papo hapo katika eneo la Ijombe  mmoja alifariki dunia mara tu baada ya kufikishwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mbeya, idadi ya majeruhi walioletwa kwa mara ya kwanza walikuwa 19.

Mkurugenzi wa Hospitali ya Rufaa Daktari Eleuter Samky amesema idadi ya waliokufa imeongeza na kufikia 13 na majeruhi na kufikia 20.

No comments:

Post a Comment