Tuesday, June 5, 2012

MBEYA UPDATE: PRODUZA WA RINGTONE YA "KITALE" ATAKA MAWAZO KWA VIDEO INAYOTARAJIA KUTOKA HIVI KARIBUNI.


P
roduza Zest wa Jijini Mbeya amewaomba wadau wa Burudani ambao wataweza kuchangia mawazo ya ALbamu yake iliyo katika mfumo wa Picha( Video)  ili ifanye vizuri katika medani ya Muziki nchini Tanzania.

Katika mahojiano na Redio Mbeya FM mchana wa leo katika Kipindi cha Bongo East Produza huyo ambaye ametengeneza wimbo wa chipukizi Ney Lee kutoka The Vibe Band unaojulikana kwa jina la “ gitaa” amesema kadhia ya muziki nchini Tanzania inatakiwa wadau wenye kujitoa kutoa mawazo yatakayofanikisha kuwaibua Chipukizi kama yeye.

Hata hivyo amekataa kuweka bayana lini atazindua video hivyo.

Produza Zest anajulikana kwa sasa nchini Tanzania hususan jijini Dar es Salaam kwa “ringtone” ya “kitale” inayotumiwa na watu wengi kwa sasa jijini humo.

No comments:

Post a Comment